Kwa hisani ya wito wangu, nikiwa pamoja na waziri Catherine Kenga wa Wizara ya barabara, usafiri na kazi kwa umma katika Kaunti, tumetembelewa na uongozi wa kampuni ya Victoria, chini ya Meneja wao wa kieneo Bw. Huang Chao.
Kampuni ya Victoria ilitikwa jukumu na serikali kuu kupitia Mamlaka ya Kitaifa ya Kusimamia Barabara Kuu Nchini KeNHA, kutengeneza barabara kuu ya Mtwapa-Kilifi na kurekebisha madaraja ya Mtwapa na Mbogolo, wamenipa ripoti ya utendaji kuhusu kazi hiyo inayodhihirisha inaendelea vyema.
Kama kaunti tutaendelea kushirikiana na serikali ya kitaifa kuhakikisha miundomsingi bora katika kaunti ya Kilifi.